KUTANA NA MREMBO MWENYE MATITI MAKUBWA ZAIDI


Jina lake halisi ni Pamella Odame Watara mwenye miaka 22, alizaliwa na mama Mghana na baba Mkenya lakini kwa sasa anaishi nchini Ghana.

Pamella amekuwa kivutio kikubwa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo licha ya rangi na sura nzuri aliyojaliwa, Pamella pia amebarikiwa kuwa na matiti makubwa yasiyo ya kawaida, kitu ambacho kinamfanya kila anapopita aache gumzo.

Matiti hayo yenye size ya 34D ambayo ni moja ya size kubwa zaidi, yamekuwa yakimpa wakati mgumu kwa siku za nyuma kutokana na kuchekwa na wenzake, lakini sasa ameamua kuyatumia kama kitega uchumi na kumuingizia pesa.

“Nilipokuwa mdogo mama yangu alikuwa anayabana kwa nguo, walishanipeleka hata hospitali kutafuta suluhu kutokana na yalivyokuwa yanakua, nilikuwa naona aibu sana lakini ninavyokua nimezoea”, alisema Pamella alipokuwa akihojiwa na moja ya mitandao nchini Ghana.
Mara nyingi watu wenye matiti makubwa ya size hiyo huwa wamefanya upasuai wa kuyaongeza, na mara chache sana huwa ya asili kama yalivyo ya Pamella.

Hivi sasa Pamella amekuwa akitumika sana kama 'video vixen' kwenye kazi mbali mbali za wasanii nchini humo, akiwemo rapper mkubwa kutoka Ghana Sarkodie.

“Wakiniona nimetokea kwenye video hivi nikipita tu, watu hutaka kuangalia zaidi huyu msichana mwenye matiti makubwa”, amesema Pamella.

Hivi sasa msichana huyo anasoma katika chuo cha Wisconsin kilichopo Accra Ghana akijikita kwenye masuala ya Marketing, huku akijihusisha na masuala ya uanamitindo kwenye mitandao ya kijamii, na kumfanya aingize mkwanja mrefu zaidi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527