BILIONI 18 KUKARABATI UWANJA WA NDEGE WA SONGWE

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya, unatarajia kutumia Sh bilioni 18 kwa ajili ya ukarabati mkubwa.

Hayo yameelezwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila (pichani) wakati wa mapokezi ya ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) aina ya AIRBUS A 220-300 ambayo imeanza safari zake za Dar es Salaam kwenda Mbeya

Alisema mbali na uwanja huo, kuendelea kutumika kwa ndege mbalimbali,imeelezwa bado uwanja huo unahitaji kufanyiwa maboresho makubwa yatakayoendana na hadhi ya kamataifa ukiwemo ukarabati wa njia za kurukia ndege.

“Hatuna neno kuu kwa Rais, zaidi tunasema ‘asante na Mungu ambariki’, ndege hii imeleta neema kubwa hapa Mbeya, hivi karibuni uwanja huu utaanza kukarabatiwa,huo ni uamuzi wenye tija na upendo kwa Tanzania uliofanywa na Rais wetu, John Magufuli,”alisema.

Alisema hatua stahiki zitachukuliwa kwa baadhi ya watumishi na watu wote waliohusika na upotevu wa mabilioni ya fedha wakati wa ujenzi wa uwanja huo ambao hadi sasa kiwango chake hakina ubora unaostahili.

Hata hivyo, wakizungumzia ujio wa ndege hiyo baadhi ya wakazi wa Jiji la Mbeya, walimuomba rais kuangalia njia mbadala itakayosaidia kupunguza gharama za usafiri huo wa
anga ili kila mmoja aweze kumudu hasa wasafirishaji wa mizigo na mazao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527