NDEGE YAANGUKA NA KUUA WATU 15


Watu 15 kati ya 16 wamekufa baada ya ndege ya mizigo kuanguka magharibi mwa mji mkuu wa Iran jana kufuatia hali
mbaya ya hewa.

Jeshi la Iran limesema ndege hiyo ya kijeshi aina ya Boeing 707 ilianguka karibu na uwanja wa ndege wa Fath uliopo katika jimbo la Alborz nchini humo.

Mhandisi wa ndege hiyo, ndiye pekee aliyenusurika na alikimbizwa hospitali.

Taarifa ya jeshi imetolewa baada ya mkanganyiko kuhusu mmiliki wa ndege hiyo.

Mapema msemaji wa mamlaka ya anga ya Iran alikiambia kituo cha televisheni cha serikali kuwa ndege hiyo ni mali ya Kyrgyzstan huku msemaji wa uwanja wa ndege wa Manas nchini Kyrgyzstan akisema inamilikiwa na Payam, shirika la ndege la Iran.

Kulingana na kituo hicho cha televisheni timu ya wataalamu tayari imepelekwa kwenye eneo hilo la ajali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527