KATIBU MKUU AWATAKA WATANZANIA KUJIANDAA KUIPOKEA SERIKALI MPYA YA CHADEMA 2020



Katibu Mkuu wa Chama cha Deokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji amewataka watanzania pamoja na dunia kujiandaa kuipokea serikali mpya chini ya chama anachokiongoza.


Dkt. Mashinji ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, akisisitiza wananchi kuielewa na kuipokea sera mbadala ya chama hicho.

"Pokeeni Sera Mbadala na jiandaeni kuipokea Serikali mpya inayoongozwa na CHADEMA baada ya October 25, 2020," amesema Dkt. Mashinji.

Aidha kiongozi huyo ametoa ujumbe kwa watu wasiopenda siasa kwa kuwakumbusha kwamba siasa ni utaratibu mzima wa kufanya maaamuzi katika jamii hivyo waipende na wasiichukie.

"Wasiopenda siasa, waambieni hivi “siasa ni utaratibu mzima wa kufanya maamzi katika jamii au kundi fulani la watu ikiwemo familia, na pili, ni matumizi ya mamlaka katika kutekeleza maamzi hayo. Tafadhari Watanzania wenzangu tuipende, tuifanye na tuiishi Siasa" Dkt. Mashinji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post