MSTAAFU ADAIWA KUUAWA KWA KUCHOMWA MKASI NA 'HOUSE BOY' WAKE


Tunsume Sakajinga (60), mkazi wa wilayani Temeke jijini Dar es Salaam ameuawa baada kupigwa na kitu kizito kichwani kisha kuchomwa na mkasi shingoni na mtu anayedaiwa kuwa kijana wake wa kazi za nyumbani.

Msemaji wa familia ambaye ni kaka wa marehemu, Kisa Mwankusye amelieleza Mwananchi kuwa mauaji hayo yametokea juzi Januari 12, 2019 saa tano asubuhi na kwamba marehemu alikutwa amechomwa mkasi shingoni na kupigwa na kitu kizito kichwani.

“Tulipata taarifa hizo saa tano asubuhi, jambo hili linaumiza sana kwa sababu lipo chini ya mikono ya polisi tunawaachia wao,” amesema Mwankusye.

Amesema dada yake alistaafu Desemba 31, 2018 na kwamba nyumbani alikuwa akiishi na kijana huyo.
Na Tumaini Msowoya, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527