BIBI ANUSURIKA KUFA AKIPAMBANA NA MAMBA AKIOGA ZIWA VICTORIA

Mkazi wa kitongoji cha Mwibale wilayani Serengeti, Chibona Matoyo (64) akihojiwa na Mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Daniel Makaka (kushoto) baada ya bibi huyo kunusurika kifo kufuatia kushambuliwa na mamba alipokuwa akioga ndani ya Ziwa Victoria, wilayani humo.


 Chibona Matoyo (64), mkazi wa Kijiji cha Kanyala Wilaya ya Sengerema, Mara amenusurika kifo baada ya kujeruhiwa na mamba wakati akioga katika Ziwa Victoria.

Katika tukio hilo lilitokea Alhamisi iliyopita, Chibona alivunjika mikono na kujeruhiwa paji la uso na sasa anapatiwa matibabu kwenye Kituo cha Afya Mwangika, Buchosa wilayani humo.

Akizungumza na Mwananchi jana, mama huyo mwenye watoto watano na wajukuu tisa, alisema wavuvi ndio waliookoa maisha yake baada ya kupiga kelele akiomba msaada.

“Walipoona napiga kelele walifika eneo la tukio na kunikuta napambana na mamba, walinisaidia kujinasua, walifanikiwa,” alisema.

Baada ya kupata taarifa za tukio hilo, mume wa Chibona, Ernest Majula (81) aliangua kilioakisema mkewe amepata kilema na kuiomba Serikali kuchukua hatua kuwadhibiti wanyama hao.

Mtoto wa mama huyo, Agnes Majula alisema wamekuwa na mazoea ya kwenda kuoga ziwani wakiamini kuwa kufanya hivyo ni vizuri zaidi kuliko majumbani mwao.

Daniel Makaka - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527