HII HAPA ORODHA YA WASANII WATAKAO PERFORM SHOW YA FUNGA MWAKA NA KING KIBA

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Salehe Kiba alimaarufu Alikiba ameweka wazi orodha ya wasanii watakaoperform katika show yake ya funga mwaka na King Kiba.

Katika Orodha hiyo wamo Mr Blue, Mwana Fa,Barnaba classic, Nuh Mziwanda, The Mafikh, Billnas, na kundi lake la The Kings music, na wengineo wengi ambapo show hii itafanyika katika ukumbi wa Next door Arena Masaki jijini Dar Es Salaam.

Kiba amewasisitiza watu kuwahi kwa ajili ya kwenda kupata burudani nyingi hasa kutoka kwa mkongwe wa Bongo fleva Mwana Fa. Alikiba aliandika hivi kuhusu Mwana Fa:-

“Labda siku nyingi hujamuona @mwanafa kwenye jukwaa. Unahitaji kusikia mashairi yake ya kitambo na ngoma kali za hapo juzi kati kama #AsanteniKwaKuja#Sielewi#DumeSurualina nyingine.

Kiu ya burudani za Falsafa itakatwa Jumamosi hii pale Next Door Arena kwenye #FungaMwakaNaKingKiba. Hakikisha unanunua tiketi yako mapema.

Bila shaka unyunyu wa @fynbyfalsafautapatikana pale pia.
#mofayabyalikiba
#FungaMwakaNaKingKiba
#KingKiba”
Advertisement

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post