RAIS MAGUFULI ASHIRIKI IBADA NA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MERCY ANNA MENGI DAR


Jeneza lenye mwili wa marehemu likiingizwa kanisani katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu Mama Mercy Anna Mengi katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018. Rais Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli walishiriki.
Watoto wa marehemu Regina na Abdiel Mengi wakiingia kanisani katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu Mama Mercy Anna Mengi katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018. Rais Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli walishiriki.
Rais Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu Mama Mercy Anna Mengi katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018.
Rais Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwapa pole wafiwa baada ya kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu Mama Mercy Anna Mengi katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018.

Picha na IKULU

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527