JESHI LA POLISI DAR LAINGIZA BILIONI 2.74 KWA MAKOSA YA BARABARANI

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amesema Makosa mbalimbali ambayo yanafanywa na wanaoendesha vyombo vya moto barabarani yamesababisha Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kupata zaidi ya Sh.Bilioni 2.74.


Mambosasa aliyasema hayo jana ambapo alifafanua kuwa jeshi hilo linaendelea na operesheni ya kuwasaka madereva wa magari na watumiaji wa vyombo vya moto ambao hawazingatii sheria ya usalama barabarani.


Alisema katika operesheni hiyo wamefanikiwa kukamata magari madogo,maroli, pikipiki na daladala ambapo wahusika wametozwa faini ambapo zaidi ya Sh.Bilioni 2.74 zimepatikana.


Kamanda Mambosasa amewawataka watu ambao wametozwa faini za barabani kulipa kwa wakati kwani kuna tabia ya kulimbikiza deni na wataendelea kuwasaka wadaiwa wote na iwapo watashindwa gari litachukuliwa na kuwekwa Polisi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527