RAIS MAGUFULI AWAONYA WAKURUGENZI

Rais John Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua kwa wakurugenzi wanaowanyima haki zao wafanyakazi kwa kuwahamisha bila kuwalipa posho ya uhamisho.


Ameyasema hayo mkoani Iringa leo katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani, ambayo kitaifa yamefanuika mkoani humo.


“Ukimuhamisha mtumishi mlipe fedha yake kabla ya kumuondoa na hili nalisema kwa mara ya mwisho sitarudia tena kulizungumza hilo katika maisha yangu.


“Leo nimeona bango jingine nafikiri chama cha walimu kinachosema wao wanaendelea kuhamishwa bila kulipwa fedha za uhamisho, najua viongozi wanaosimamia wizara zinazohamisha wako hapa, kama kuna mtu yeyote anahamisha bila kulipa huyo ni jeuri na dawa yake ni kumtoa”, amesema Rais Magufuli.


Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli amewataka wananchi wa Iringa na Njombe kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa Ukimwi kutokana na mikoa hiyo miwili kuongoza kwa ugonjwa huo nchini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527