KISA CHA MWANAMKE KUANGUA KILIO MBELE YA RAIS MAGUFULI

Rais John Pombe Magufuli ametoa agizo kwa Mkuu wa Mkoa Iringa pamoja na RPC mkoani humo kumpatia msaada mwanamama Salmakoni Sanga ikiwa ni pamoja na kumpima kama kweli ametolewa kizazi baada ya kudai kushambuliwa na kijana aliyemtaja kwa jina la Mussa.


Rais Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kumaliza kuhutubia katika sherehe za Mei Mosi mkoani Iringa ambapo mama huyo alijitokeza na kumlilia Rais Magufuli ampatie msaada kutokana na kunyimwa haki yake mahakamani.


Mama huyo amesema kwamba tukio lake la kushambuliwa na Bw. Mussa lilifanyika mwaka jana ambapo shambulio lilimfanya apoteze kiumbe kilichopo tumboni hali iliyompelekea kutolewa kizazi.


Hata hivyo mama huyo amesema kwamba pamoja na maumivu aliyosababishiwa na kijana huyo, bado mahakama ilimuachia huru mtu huyo na yeye akiamini kwamba alidhulumiwa haki yake na mahakama ya mkoa huo.


Akitoa maagizo, Rais Magufuli amemtaka RPC Iringa Juma Bwire na Mkuu wa Mkoa Bi. Amina Masenza kumtafuta kijana huyo na kumfungulia mashtaka upya hata kama alishinda kesi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527