TUCTA WAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUONGEZA MSHAHARA KIMA CHA CHINI

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) limemuomba Rais John Magufuli kuangalia namna ya kuongeza mshahara wa kima cha chini angalau kisiwe chini ya Sh250, 000.


Hayo yamesemwa leo Mei Mosi na Katibu Mkuu wa Tucta, Dk Yahaya Msigwa wakati wa sherehe za wafanyakazi, zinazoadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Samora mkoani Iringa, ambapo Mgeni Rasmi ni Rais John Magufuli.


Amesema maisha kwa walio wengi yanakuwa magumu kutokana na kupanda kwa bei za vitu muhimu ikiwemo vyakula na huduma za msingi za maisha.


“Tunaomba Rais wetu kima cha chini kisipungue 250,000 kwa mwezi , lakini pia tunaiomba Serikali kubuni vyanzo vingine vya mapato ili kuongeza wigo wa utoaji huduma kwa watumishi au wafanyakazi, kuna mfanyakazi anapata Sh100,000 hii haitoshi kitu kwa mtu mwenye familia yenye watoto wanne,” amesema Dk Msigwa.


Aidha alitoa wito kwa Serikali kuangalia upya namna ya kubuni vyanzo vingine vya mapato ili kupunguza machungu kwa wafanyakazi kwani wanakatwa kodi kubwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527