POLEPOLE ATISHIA KUNG'OA KIONGOZI MKUBWA WA CHADEMA DAR

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole ametishia kung’oa kiongozi mkubwa wa Chadema ndani ya mkoa wa Dar es salaam.


Ameyasema hayo mara baada ya madiwani wawili wa CHADEMA kuachia ngazi Mjini Iringa, ambapo amesema kuwa hoja za madiwani hao wanakimbia ubabe wa mchungaji Msigwa ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo.


"Leo Madiwani wengine wawili wamehama na kujiunga na CCM. Ukiwasikiliza kilichowaondoa ni Uongozi Mbovu na Ubabe pale Iringa Mjini. Nasikia wameambiwa "never outshine your master". Mimi nilidhani "masta" ni wananchi kumbe ni "pasta". Ukitukana tusi moja Kiongozi mmoja nachomoa DSM " Ameandika Polepole


Siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la viongozi wa kisiasa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA) kuhamia chama tawala cha CCM.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527