HAJI MANARA AACHIWA HURU NA KAMATI YA NIDHAMU TFF KUITUMIKIA SIMBA SC




Wote wanaofatilia soka mnajua kwamba Mkuu wa kitengo cha Habari wa Simba SC Haji S. Manara alipewa kifungo kama adhabu na TFF siku zaidi ya 70 zilizopita lakini leo imekuja habari mpya kuhusu kifungo hicho.

Habari yenyewe ni kwamba Haji Manara ameachiwa huru na kamati ya nidhamu ya TFF na sasa ataendelea na majukumu yake kama kawaida.

Simba SC imethibitisha taarifa hiyo kwa kusema “Kamati ya nidhamu ya TFF imemuachia huru mkuu wa kitengo cha Habari wa klabu ya Simba Haji Manara sasa kuendelea na majukumu yake kama kawaida.”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527