Katika hali isiyo ya kawaida, mfungwa mmoja aliyetambulika kwa jina la Troy Smith amemuomba Jaji wa mahakama ya Canterbury, Uingereza amuongeze kifungo cha miezi sita jela ili aweze kumalizia kozi alizokuwa akizipitia wakati akiwa jela.
Mwanaume
huyo mwenye miaka 41, August mwaka jana alifikishwa mahakamani hapo kwa
kosa la kuvamia na kumpiga vibaya mtu mmoja na kumsababishia maumivu na
kutoka damu kwenye ubongo.
Hata
hivyo mtu huyo alionesha jeuri ya aina yake baada ya kukamatwa na
kutupwa katika selo za polisi. Jamaa alijisaidia haja ndogo kwenye
kwenye selo za polisi na inaripotiwa kuwa alimtemea mate afisa wa
polisi.
Baada
ya kufikishwa mahakamani alikubali makosa yote na kufungwa jela kwa
kipindi cha miezi sita. Lakini baada ya kutoka, Smith akishirikiana na
wakili wake walimuomba Jaji amuongeze kifungo/amrudishe jela ili
akamalizie kozi yake ambayo alidai ingemsaidia sana kwa maisha yake ya
baadae.
“Ningependa
unipe miezi mingine sita jela kwa sababu nitaweza kumalizia kozi
nilizokuwa nazipitia ambazo zitanisaidia kuelekea katika maisha yangu ya
baadae.” Alisema Smith.
Kwa mujibu wa gazeti ya Kent, Jaji alikubalina na ombi hilo na kumrudisha jela kwa kipindi cha miezi sita mingine.
Post a Comment