Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, amefanya kikao kazi na watumishi wa taasisi hiyo kutoka kampasi zote, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, umoja na mshikamano katika kufanikisha malengo ya taasisi.
Akifungua kikao hicho, Dkt. Maulid mesema kuwa watumishi wanapaswa kuwajibika kikamilifu katika nafasi zao huku wakidumisha mshikamano ili kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi.
“Tunapaswa kuwajibika kwa nafasi zetu kwa kuwa wamoja na wenye mshikamano ili kuleta tija katika utimizaji wa malengo ya taasisi,” amesema Dkt. Maulid.
Katika kikao hicho, watumishi wapya waliojiunga na ADEM kutoka taasisi mbalimbali walipata fursa ya kujitambulisha, ambapo waliaswa kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kujituma ili kuchangia maendeleo ya taasisi hiyo.
Kwa upande wake, Dkt. Lucas Mzelelela amesisitiza umuhimu wa watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma kwa kufanya kazi kwa bidii na nidhamu wakati wote wawapo kazini.
“Kila mtumishi anapaswa kutumikia kiapo chake cha utumishi wa umma kwa kuwajibika ipasavyo na kuwa na nidhamu ya kazi kwa muda wote wawapo kazini,” amesema Dkt. Mzelelela.















Social Plugin