Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Shinyanga, Emmanuel Ntobi, amejiunga rasmi na Chama cha ACT Wazalendo, ambapo amepokelewa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu.
Akizungumza katika hafla fupi ya kuwapokea wanachama wapya, Ado Shaibu amesema chama hicho kinaendelea kupokea wapiganaji wa demokrasia kutoka pande mbalimbali za nchi wanaovutiwa na dira ya ACT Wazalendo.

Mbali na Ntobi, Ado Shaibu pia alimtambulisha Glory Tausi, ambaye naye ni kada mwandamizi wa CHADEMA aliyeamua kujiunga na ACT Wazalendo.
Ado amesema wote wameandika barua rasmi za kujiunga na chama hicho, na chama kimewakaribisha kwa mikono miwili.
Ado Shaibu pia ametoa wito kwa watu wengine wanaotamani kujiunga na ACT Wazalendo kujitokeza, akisema nafasi bado zipo wazi kwa wapigania mabadiliko wenye dhamira ya kweli.
Social Plugin