Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

NDUMBARO AHAMASISHA UUNGWAJI MKONO KWA SONGEA UNITED KABLA YA MECHI DHIDI YA COSMO

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma 

Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Mheshimiwa Damas Ndumbaro, ametoa kauli kuhusu mchezo wa kesho Jumapili tarehe 11 Mei 2025 kati ya Songea United na Cosmo Politan kutoka Dar es Salaam. 

Waziri Ndumbaro amesisitiza umuhimu wa mchezo huo na kueleza kuwa Cosmo ni timu iliyowahi kushinda ubingwa mara mbili mbele ya vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga, hivyo mchezo huo unatarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa.

Aidha, Waziri Ndumbaro ameisifu timu ya Songea United kwa kuonesha kiwango kizuri ilipocheza dhidi ya Yanga, licha ya kufungwa kwa bao moja kwa sifuri katika mchezo uliojaa ushindani mkali na tuhuma za upendeleo. 

Amesema kiwango hicho kinaonesha kuwa Songea United ina uwezo mkubwa wa kushindana na timu kubwa nchini, hivyo inahitaji kuungwa mkono zaidi na jamii ya Songea.

Katika jitihada za kukuza na kuimarisha timu hiyo, Waziri Ndumbaro ametoa wito kwa wenyeviti wa mitaa kuanzisha matawi ya Songea United katika kila mtaa. 

Ameeleza kuwa kuanzishwa kwa matawi hayo kutasaidia kuongeza wanachama, kukuza uchumi wa timu, na kuimarisha mshikamano wa mashabiki wa nyumbani kwa lengo la kuinua soka la Songea.

 Waziri Ndumbaro amewataka wananchi wa Songea kuonesha uzalendo kwa kuvaa jezi za Songea United badala ya kuvaa jezi za timu zingine kama Simba na Yanga. 

Amesisitiza kuwa mafanikio katika soka na maendeleo ya timu ya mkoa yanatokana na mshikamano, ushirikiano na kujitambua kama jamii inayojali maendeleo ya michezo kwao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com