Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

RAIS SAMIA APOKEA UJUMBE WA HAYATI PAPA FRANCISKO KWA WATANZANIA

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amepokea kwa unyenyekevu na shukrani ujumbe wa hayati Papa Francisko aliouandika kwa ajili yake, kwa nchi yetu na kwa Watanzania wote.

Ujumbe huo uliandikwa na hayati Papa Francisko siku chache kabla ya kuaga dunia na ulikabidhiwa kwa Rais Samia na Balozi wa Vatican hapa nchini, Askofu Mkuu Angelo Accattino.

Kupitia ujumbe wake kwa umma, Rais Samia amesema:

"Kwa unyenyekevu na shukrani, nimepokea ujumbe wa hayati Papa Francisko kwangu, kwa nchi yetu na kwa Watanzania wote, aliouandika siku chache kabla Mwenyezi Mungu hajamwita kwake, na kumkabidhi Balozi wa Vatican hapa nchini, Askofu Mkuu Angelo Accattino. Tuendelee kumwombea kwa Mwenyezi Mungu alale mahali pema."

Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuendelea kumkumbuka hayati Papa Francisko katika sala na kumuombea apumzike mahali pema.

Hayati Papa Francisko atakumbukwa na Watanzania kwa mchango wake mkubwa katika kuhimiza imani, amani, mshikamano, na upendo miongoni mwa watu wote duniani, hususan bara la Afrika.

Imeandaliwa na Malunde 1 blog

Rais Samia Suluhu Hassan alipokutana na Papa Francisko Februari 2024

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com