WATU SITA WAFARIKI, WENGINE WATANO WAPOFUKA MACHO BAADA YA KUNYWA POMBE


Watu sita walithibitishwa kufariki baada ya kunywa pombe haramu katika kijiji cha Kangai nchini Kenya.

Wengine watano walithibitishwa kuwa vipofu. 

Kisa hicho kilithibitishwa na Afisa Mkuu wa Afya katika Kaunti ya Kirinyaga, George Karoki, ambaye alisema kinywaji ambacho waathiriwa walinywea huenda kilikuwa na ethanol.

"Walikuwa wamekunywa pombe haramu na tunashuku kuwa lazima ilikuwa na ethanol kwa sababu aina ya ishara na dalili ambazo zimeonyeshwa kutoka kwa wagonjwa zimeonyesha kuwa walikuwa na uoni hafifu," Karoki alisema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post