MSAJILI WA HAZINA ZANZIBAR AWASHIKA MKONO WAATHIRIKA WA MAAFA HANANG’


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama akipokea mfano wa Hundi ya kiasi cha Shilingi Milioni 54.3 kutoka kwa Msajili wa Hazina wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Waheed Mohammad Ibrahim Sanya, kwa ajili ya waathirika wa Maafa ya Hanang’, Ofisini kwake Bungeni Dodoma Tarehe 9 Februari 2024.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama akipokea mfano wa Hundi ya kiasi cha Shilingi Milioni 54.3 kutoka kwa Msajili wa Hazina wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Waheed Mohammad Ibrahim Sanya, kwa ajili ya waathirika wa Maafa ya Hanang’, Ofisini kwake Bungeni Dodoma Tarehe 9 Februari 2024.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)




NA; MWANDISHI WETU – DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama amepokea mchango wa Msajili wa Hazina Kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar uliyowasilishwa kwake Februari 9, 2024 wa kiasi cha Shiliingi za Kitanzania Milioni Hamsini na Nne nukta Tatu (54.3 Milioni) kwa ajili ya waathirika ya Maafa ya maporomoko ya tope, miti na mawe yaliyotokea tarehe 3 Disemba, 2023 mkoani Manyara.

Akizungumza baada ya kupokea mfano wa hundi hiyo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma tarehe 9 Februari, 2024 Waziri Mhagama ameishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kuguswa kwa kiasi kikubwa na maafa yaliyotokea Hanang’ ambayo yamesababisha watu kupoteza maisha na mali zao na kuongeza kusema kuwa, baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kutangaza hali ya hatari kabla ya kutokea kwa maafa hayo, Kamati za Maafa za Mikoa zilikuwa zimeshajipanga kwa kutoa elimu na tahadhari.

Aliendelea kusema kuwa, kwa sasa Serikali inatekeleza ahadi yake ya kuwajengea nyumba waathirika wa maafa hayo na maandalizi ya awali yameshaanza kutekelezwa.

Aidha, Waziri Mhagama ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari kwa msimu huu wa mvua za el nino zinazoendelea na kuongeza kusema kuwa msimu wa mvua za masika unakuja hivyo kila mmoja aendelee kuchukua tahadhari.

“Mmefanya jambo kubwa kuungana nasi kwa kuwashika mkono waathirika wa maafa ya Hanang’ kipekee ninawashukuru sana kwa moyo huu na mmeonesha faida za Muungano wetu na mashirikiano tuliyonayo katika hali zote, iwe furaha au majonzi kama haya, ninaahidi kuendelea kutoa ushirikiano nanyi,” alisisitiza Mhe Mgahama.

Kwa Upande wake Msajili wa Hazina wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Waheed Mohammad Ibrahim Sanya alisema, Ofisi yake iliguswa na maafa yaliyotokea Hanang’ na kuona kuna kila sababu ya kuungana kwa kuwashika mkono waathirika hao kwa kutoa mkono wa Pole.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post