WAZIRI UMMY AITAKA WIZARA YA AFYA KUWA NA MPANGO WA HUDUMA ZA METHADONE KATIKA KILA HALMASHAURI NCHINI


Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza 
wakati halfa ya kukabidhi  vifaa tiba,vitendanishi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo ambapo zoezi hilo lilikwenda sambamba na kugawa vifaa ujasiriamali kwa ajili ya vijana waliokuwa wakipata huduma ya methadone na kuhitimu kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga Kanali Maulid Surumbu na kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shillow kulia ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Doroth Lema 
KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Tanga Kanali Maulid Surumbu akizungumza wakati wa halfa hiyo kushoto ni Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kulia ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga  Doroth Lema ambaye pia ni Mratibu wa Huduma za Mama na Mtoto Mkoa wa Tanga

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katika akikate utepe wakati wa halfa hiyo kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga Kanali Maulid Surumbu kushoto ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Doroth Lema 
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo Dkt Naima Yusuf aliyevaa hijabu akifuatilia kwa umakini matukio mbalimbali katika halfa hiyo kulia ni Katibu wa Hospitali hiyo Abas Mlawa
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katika akiwa kwenye picha ya pamoja 




Na Oscar Assenga, TANGA.

WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu ameielekeza Wizara ya Afya kuweka mpango wa kuhakikisha huduma za Methadone zinakuwepo katika kila Halmashauri zote 184 nchini ili kuwapunguzia wahitaji umbali wa kuzipata.

Ummy aliyasema haya leo wakati akikabidhi vifaa tiba,vitendanishi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo ambapo zoezi hilo lilikwenda sambamba na kugawa vifaa kwa ajili ya vijana waliokuwa wakipata huduma ya methadone na kuhitimu.

Vifaa hivyo vilikabidhiwa sambamba vile vya ujasiriamali kwa ajili ya waraibu waliomaliza matibabu yao na walipo hatua za mwishoni kupata matibabu ili waweze kupata vifaa vya ujasiriamali zitakavyowasaidia katika maisha yao watakaporudi kwenye maeneo yao

Alisema kwa sababu watu hao nauli wanapata wapi na kila siku wizara ya afya wataka kuona mpango wenu mwakani wanaongeza vituo vingapi na mwaka kesho ili mwaka 2025 wawe wamezifikia Halmashauri zote nchini.

“Kwani kuna watu wanatoka Pangani,Handeni ,Muheza Korogwe hao watu nauli kila siku wanapata wapi kuja kupata dawa na kurudi jambo ambalo linakuwa ni changamoto kwao”Alisema

Akizumza baada ya kukabidhi vifaa hivyo alisema vitawasaidia kuweza kujikwamua kiuchumi lengo likiwa ni kuweza kufanya shughuli za kujiingizia kipato halali na hivyo kuachana na kufikiria kurudi kwenye matumizi ya dawa hizo.

Vifaa walivyokabidhiwa vifaa kwa ajili ya kutenegeneza maridhisha ya milango seti mbili thamani ya Milioni 38 na vyerahani 10 vyenye thamani ya Milioni 48 pia watakwenda kutatafuta shule ambazo watakuwa wakiwashonea wanafunzi kila mwaka.

Aidha pia watakabidhi mashine mbili za matofali kwa siku zenye thamani ya Milioni 70 ambapo alimtaka Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga tenda ya kwanza oda ipewe watu wa MAT ili kuweza kulisaidia kundi la vijana waliokuwa wakitumia dawa zaa kulevya

Alisema msaada huo ni sehemu ya kuwainua kiuchumi ili washiriki kwenye shughuli za kimaendeleo na hatimaye wasirudi kule walipotoka katika matumizi ya dawa za kulevya.

Aidha Waziri Ummy alisema kwamba kutokana na uwepo wa maombi ya baadhi yenu kuona eneo la kuoshea magari watapeleka mpango huo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo,Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha Mount Meru na ile ya Mkoa wa Dodoma Utenga mashine za kuoshea magari zenye thamani ya milioni 90 .

Alisema pia katika mwezi Desemba mwaka huu watanunua vifaa vya saluni za kiume na kike lengo likiwa ni kuinua kipato cha vijana waliopo kwenye hali nzuri baada hya kupata huduma ya methadone wanaamini wataweza kujisaidia na wanawaomba wasirudi kule walipotoka.

“Ndugu zangu vijana wa Tanga ambao bado hamjaingia kwenye matumizi ya dawa za kulevya msiingie huko lakini nafurahi kuna taasisi zinaelimisha vijana wa Tanga naomba waongeze nguvu katika hili ili kuwaepushga vijana na utumiaji”Alisema

Waziri Ummy pia alizitaka Taasisi ambazo zimekuwa zikitoa elimu kwa vijana viwafikie vijana kwenye shule za Msingi na Sekondari kuwahamasisha wasijiingize kwenye matumizi ya dawa za kulevya.

“Tunaomba nyie muwe mabalolozi tuwe na mpango wa kupita kwenye shule za Msingi na Sekondari na tunaandaa mambo mbalimbali kuhakikisha tunatoa elimu kwa wanafunzi”Alisema

Kuhusu ukatishaji wa matibabu kwa waraibu.

Waziri Ummy alitumia halfa hiyo kuwataka waraibu wanaotumia dawa za kupunguza makali ya dawa za kulevya kuhakikisha hawakatishi matibabu mpaka watakapoambiwa wapo sawa.

“Kwa maana kuna ambao mnapata matibab na kuamua kuacha wenyewe hapana msikatishe matibabu mpaka mtakapoambiwa mpo sawa lakini pia niwatake vijana waliopo majumbani tuache kujiingiza kwenye matumizi ya dawa hizi”Alisema

Alisema kwamba kukabidhiwa kwa vifaa hivyo inaonyesha namna Serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu inavyowajali na kuwathamani watu wa aina zote ikiwemo wanyonge.

Alisema kitendo hicho ni Imani na huduma ya Rais Dkt Samia Suluhu anawajali watu wake na kuwapenda na vifaa hivyo ni kwa ajili ya kutengeneza madirisha ya milango seti mbili zenye thamani ya sh Milioni 38 .

“Hivyo niombe Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shillow kwamba wakati tunajenga,ofisi za kata ,oda ya kwanza watoe kwa vijana hao ambao leo wanapewa vifaa hivyo ili waweze kujikwamua kiuchumi”Alisema

Vifaa walivyokabidhiwa ni vyerahani 10 vyenye thamani ya Milioni ambapo watatafuta shule ambazo watakuwa wakiwashonea wanafunzi kila mwaka watakabidhi mashine mbili za matofali 500 kwa siku zenye thamani ya Milioni 156.

Alisema kupitia Madiwani kuhakikisha tenda za ujenzi katika maeneo mbalimbali Jijini huo kuwaangalia namna ya kjuwkwenye mashine amemuomba meya na madiwani wanafanya ujenzi mara nyiny wanaomba tenda ya kwanza wapewa watu wa MAT.

Awali akizungumza katika Halfa hiyo Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga Kanali Maulid Surumbu alimpongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuangalia makundi yote kwa namna ya kipekee na Waziri Ummy kwa kumsaidia vizuri Rais.

Kanali Maulid ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Mkinga alisema watapokea vifaa hivyo vitavyosaidia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga- Bombo ambapo alisema vikitumia vizuri vitaongeza ufanisi wa utoaji wa huduma ya Afya kwa wananchi wa Tanga.

Sambamba na kukabidhi dawa za tiba asili ambapo alisema ni ukweli tangu dunia imeanza wamekuwa wakipata tiba asili na zile za kisasa lakini kwa muda mrefu zilikuwa hazipewe kipaumbele .

Hivyo niwapongeze wizara kwa kutekeleza hilo wakiwatambua na kuwathamani wanaimani kwa miaka ijayo watanzania watatengeneza dawa zinazofanana na wenzao waliotutangulia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post