TMA YATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA ZENYE HATARI YA MAFURIKO


Mvua

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa tahadhari ya uwezekano wa kunyesha mvua kubwa kuanzia leo Jumatano Novemba 22 hadi Novemba 25 ambazo huenda zikasababisha mafuriko kwa maeneo machache ambayo yanaweza kusababisha vifo.

Mvua hizo zinatarajiwa kunyesha katika Mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara, Tanga na visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.

Kupitia taarifa ya Mamlaka iliyotolewa jana Jumanne Novemba 21, 2023, imetaja athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na baadhi ya barabara kutopitika kutokana na mafuriko pamoja na vifo kwa siku hizo, hivyo wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari.

Via EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post