MBUNGE UMMY MWALIMU ACHANGIA MILIONI SITA NA LAKI TATU (6,300,000) KUWEZESHA WAJASIRIAMALI NA VIJANA NGAMIANI KATI JIJINI TANGA

 











Mbunge wa Tanga Mjini, Mhe Ummy Mwalimu leo tarehe 16/07/2023 ametembelea Kata ya Ngamiani Kati ambapo pia amechangia kiasi cha shilingi milioni sita (6,000,000/-) kwa vikundi vitatu vya Wajasiriamali ambavyo ni Nguvu Kazi kilichopo barabara 12 Mnadani, Mtaa wa Makoko; Kikundi cha Kuonda Mai cha Wafanyabiashara wa kuku kilichopo Sokoni Ngamiani na Kikundi cha Wazee kilichopo mtaa wa Maua. Kila kikundi, kimepatiwa kiasi cha shilingi milioni 2. 

Aidha, Mh Mbunge amechangia shilingi laki 3 kwa ajili ya kukarabati Sehemu ya kufanya mazoezi ya ngumi kwa vijana katika mtaa wa Karafuu.

Mhe Ummy ameeleza kuwa licha ys majukumu ya kitaifa aliyonayo ataendelea kutimiza wajibu wake kikamilifu wa kuwatumikia wananchi wa Tanga Mjini hususani kutatua kero za maendeleo ya wananchi kupitia fedha za Serikali Kuu, Fedha za Halmashauri pamoja na mshahara wake na posho. 

Akizungumza baada ya kupokea mchango huo kwa niaba ya vikundi vingine, Ndugu Sadik Ali Mwenyekiti wa Kikundi cha Nguvukazi alimshukuru Mhe Mbunge kwa kuendelea kuwajali wananchi wake.

Katika ziara hii, Mhe Ummy aliongozana na Mhe Habibu Mpa, Diwani wa Kata ya Ngamiani Kati, Mhe Fatuma Kitogo, Diwani wa Viti Maalum pamoja na Viongozi wa CCM ngazi ya Kata na matawi.

Imetolewa na;-
Ofisi ya Mbunge, Jimbo la Tanga Mjini
16/07/2023

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post