MTOTO ALIYEDAIWA KUFARIKI NA KUZIKWA AKUTWA AKIWA HAI


Wakazi wa Kijiji cha Salong’we kilichopo wilayani Magu mkoani Mwanza wamekumbwa na taharuki baada ya mtoto aitwaye Mabilika Wilson aliyefariki na kuzikwa tarehe 17 mwezi huu kupatikana akiwa hai katika Kijiji cha Mwangika wilayani Kwimba mkoani humo.

Wilson Bulabo ni baba mzazi wa mtoto huyo amesema ni kweli mtoto wake huyo aliumwa kwa siku mbili na kufariki hatimaye wakamzika lakini alipoenda kumuangalia huyo mtoto aliyeonekana Kijiji cha Mwangika alimgundua kuwa ndiye mtoto wake aliyezikwa wiki chache zilizopita.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amefika katika Kijiji hicho na kushuhudia kaburi likifukuliwa kwa ajili ya taratibu za uchunguzi wa tukio hilo ambapo amewataka wakazi wa Kijiji hicho na vijiji vya Jirani, kuwa watulivu kipindi ambacho uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.

Via EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments