BODI YA WAKURUGENZI TBS YAZIPONGEZA OFISI ZA TBS KANDA YA KASKAZINI KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE IPASAVYO


BODI ya Wakurugenzi Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetembelea ofisi za Shirika hilo zilizopo kanda ya Kaskazini kuona kazi zinaendaje na kama kuna kitu cha kuboreshwa kiboreshwe ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabiri.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof.Othuman Chande amesema kuwa watafanya kazi kwa nguvu moja lengo ni kuhakikisha wanasimamia sheria ya ubora wa bidhaa hasa kwenye maeneo ambayo bidhaa zinapita kwa wingi.

Amesema sehemu zote walizopita wamekuta kazi zinakwenda vizuri japokuwa kuna changamoto ndogondogo ambazo wameomba kuzishughulikia ili Shirika hilo liendelee kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora Bw.Lazaro Msasalaga amesema wamekuwa na  utaratibu wa kufuatilia bidhaa sokoni ziwe za kutoka nje au za kutoka ndani ya nchi ambapo wanapita kwenye masoko na maduka wanazinunua na kwenda kuzipima kujihakikishia kwamba kweli zinaendelea  kukidhi ubora na usalama.

"Mifumo yote inasimamia vizuri nashukuru wadau mbalibali wanatoa ushirikiano na tuendelee kuomba wadau wa kutosha kwasababu TBS haiwezi kuona kila kitu na kila mahali nchini kwahiyo wadau wengi wanatupatia taarifa za msingi na sisi tunakuwa tunazifuatilia na kuchukua hatua za kisheria". Amesema 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments