AMUUA BIBI YAKE KISA KANYIMWA PESA


Wenyeji wa Kijiji cha Eshitimba, Kaunti ya Kakamega wametamaushwa na kifo cha ajuza wa miaka 89.

Floice Lisero, alikufa moto baada ya mjukuu wake wa kiume mwenye umri wa miaka 40, kuteketeza nyumba yake kufuatia mzozo kuhusu pesa.

Mshukiwa huyo tayari amekamatwa na polisi, na inadaiwa alimshambulia bibi yake baada ya kukataa kumpa pesa alizomuitisha.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Khwisero Samuel Kogo alithibitisha mkasa huo, akisema kwamba polisi walimuokoa mshukiwa huyo kutoka kwa wanakijiji waliojaribu kumpiga kitutu katika soko la Ebukambuli.

Kamanda huyo alisema kwamba mwanamume huyo atapimwa akili kubainisha iwapo yuko sawa au tahira, kabla ya kufunguliwa mashtaka dhidi yake.

“Ni lazima tumpeleke akapimwe akili ili kuthibitisha iwapo ako timamu au la kabla ya kumfungulia mashtaka yoyote,” Kogo alisema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments