KIJANA APOTEZA KORODANI KWENYE MAANDAMANO

Mwanaume mmoja anadaiwa kupoteza korodani zake kufuatia kichapo cha mbwa alichopokezwa katika maandamano ya kupinga mageuzi ya pensheni nchini Ufaransa.


Katika picha na video za maandamano hayo ya Alhamisi, Januari 19, zinazosambaa mtandaoni, afisa wa polisi anaonyeshwa akimpiga mwanamume mmoja mateke katikati ya miguu, na kisha kuondoka.


Mwanaume huyo anaonekana akiwa ameshika kamera. 

Wakili wa mwanaume huyo Lucie Simon alisema Jumapili, Januari 22, kuwa atawasilisha malalamishi kwa niaba ya mteja wake ambaye ni mhandisi mwenye umri wa miaka 26.


Mwanaume huyo mwenye asili ya Kihispania anaripotiwa kwamba alikuwa akipiga picha za maandamano hayo kwa hiari na kupelekea kukatwa kwa nyeti zake na polisi. 

Kulingana na wakili wake, mhandisi huyo bado yuko hospitalini na korodani zake zililazimika kukatwa kutokana na pigo kali. 

"Hii sio kesi ya kujilinda au lazima. Ushahidi uko kwenye picha tulizonazo na ukweli kwamba hakukamatwa. Bado yuko katika mshtuko na anaendelea kuuliza ni kwa nini alijeruhiwa," wakili huyo alisema.


Idara ya polisi jijini Paris ilitoa taarifa ikisema kuwa uchunguzi wa kina kuhusu kisa hicho umeanzisha na kuongeza kuwa tukio hilo lilitokea katika mazingira ya ghasia kali na ndani ya mamlaka ya polisi kuwakamata watu wenye kuzua vurugu.

 Wizara ya mambo ya ndani nchini humo ilisema kuwa takriban Wafaransa 80,000 waliandamana mjini Paris siku ya Alhamisi, kama sehemu ya maandamano ya nchi nzima kupinga mpango wa Rais Emmanuel Macron wa kuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 62 hadi 64.


Baadhi ya waandamanaji walionekana kuwarushia polisi chupa, mapipa na grunedi za moshi.


Polisi waliamua kujibu kwa kuwatupia waandamanaji hao vitoa machozi ili kuwatawanya waliozua fujo na vurugu.

Chanzo - Tuko News

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments