UHURU FM, TANCDA WAZINDUA KAMPENI YA KUKABILIANA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA.

Meya wa Jiji la Dar es salaam, Mh.Omary Kumbilamoto akiwaongoza watumishi wa Uhuru Fm pamoja na Shirikisho la vyama vya magonjwa yasioambukiza Tanzania-TANCDA kwenye Jogging katika uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara ikiwa ni njia moja wapo ya kujikinga na magonjwa yasioambukiza iliyofanyika leo Oktoba 15,2022 Jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ilala, Said Sultan Sidde akifanya usafi kwenye Zahanati ya Vingunguti katika uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara ikiwa ni njia moja wapo ya kujikinga na magonjwa yasioambukiza iliyofanyika leo Oktoba 15,2022 Jijini Dar es Salaam. Meya wa Jiji la Dar es salaam, Mh.Omary Kumbilamoto akifanya usafi kwenye Zahanati ya Vingunguti katika uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara ikiwa ni njia moja wapo ya kujikinga na magonjwa yasioambukiza iliyofanyika leo Oktoba 15,2022 Jijini Dar es Salaam. Meya wa Jiji la Dar es salaam, Mh.Omary Kumbilamoto na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ilala, Said Sultan Sidde wakipata picha ya pamoja na watumishi wa Uhuru Fm pamoja na Shirikisho la vyama vya magonjwa yasioambukiza Tanzania-TANCDA katika uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara ikiwa ni njia moja wapo ya kujikinga na magonjwa yasioambukiza iliyofanyika leo Oktoba 15,2022 Jijini Dar es Salaam. Meya wa Jiji la Dar es salaam, Mh.Omary Kumbilamoto na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ilala, Said Sultan Sidde wakipata picha ya pamoja na watumishi wa Uhuru Fm pamoja na Shirikisho la vyama vya magonjwa yasioambukiza Tanzania-TANCDA katika uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara ikiwa ni njia moja wapo ya kujikinga na magonjwa yasioambukiza iliyofanyika leo Oktoba 15,2022 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*******************

Na Mwandishi wetu, 15.10.2022

Katika kukabiliana na magonjwa yasiambukiza, Uhuru fm kwa kushirikiana na Shirikisho la vyama vya magonjwa yasioambukiza Tanzania-TANCDA, wamezindua kampeni ya kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara ikiwa ni njia moja wapo ya kujikinga na magonjwa yasioambukiza.

Kampeni hiyo imezinduliwa na Meya wa Jiji la Dar es salaam, Mh.Omary Kumbilamoto kwa kufanya maazoezi ya Jogging kuanzia Buguruni Sheli hadi Vingunguti iliyoshirikisha vikundi mbalimbali vya Jogging na kisha baadaye kufanya usafi katika Hospitali ya Vingunguti.

Katika uzinduzi wa kampeni hiyo ya magonjwa yasiyoambukizwa alikuwepo pia Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ilala, Said Sultan Sidde.

Chini ya mpango huo wa kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi zaidi ili kujikinga na magonjwa yasioambukiza, Meya wa Jiji la Dar es salaam, Kumbilamoto, ameiomba jamii kufanya mazoezi ili kujikinga ma magonjwa hayo ambayo yamekuwa ni tishio hapa nchini na Duniani kwa ujumla.

Magonjwa yasioambukiza ni pamoja na Kisukari, Saratani, Kiharusi, maradhi ya Moyo, pamoja na Figo.

Aidha, kwa mujibu wa kitabu cha TANCDA, dalili za magonjwa yasioambukiza ni pamoja na kuchoka bila sababu, kichwa kuuma, kuona kizunguzungu, kutoona vizuri, ganzi ya meno, kupumua kwa shida, moyo kwenda kwa haraka, kutokwa na damu sehemu yoyote, kukosa pumzi wakati wa kulala pamoja na vidonda visivyopona.

Kutokana hali hiyo jamii imetakiwa kufanya mazoezi mara kwa mara angalau mara tatu kwa wiki.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala, Sidde, ameishukuru Uhuru Fm kwa kuwa na kampeni hiyo ambayo amesema itasaidia jamii kujenga tabia ya kufanya mazoezi ili kuweka miili yao sawa kiafya. Naye Mhariri Mkuu wa Uhuru FM, Pius Ntiga, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Uhuru Fm, Amina Azizi, amesema kampeni hiyo itakayokuwa ikifanyika kila mwisho wa wiki itakuwa ni mwendelezo lengo pia likiwa ni kuisaidia pia jamii kubadili mtindo wa maisha hasa katika ulaji wa vyakula na kuwasisitiza kufanya mazoezi ili kjjikinga na magonjwa yasioambukiza.

"Hii ni awamu ya pili ya Jogging ya Uhuru fm, ambapo awamu ya kwanza tulijikita zaidi katika masuala ya sensa ya watu na makazi 2022, ambayo kwa kiasi kikubwa tulifanukiwa, tukaona tusiishie hapo na sasa yaani leo tumezindua tena Jogging itakayojikita katika magonjwa yasiyoambukiza, tuhamasishe jamii ifanye mazoezi" alisema Ntiga.

Aidha, Ntiga amevishukuru vikundi mbalimbali vilivyojitokeza katika uzinduzi huo ikiwemo Jogging ya Vingunguti, Miembeni, Ukonga, pamoja na Tabata veteran.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments