SIMBA SC YATOA DOZI NZITO MTIBWA SUGAR, YAICHAKAZA MABAO 5-0


*****************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Simba imeamua kuifanyia ukatili Mtibwa Sugar baada ya kuinyeshea mvua ya magoli 5-0 na kuondoka na ushindi huo muhimu wa ligi kuu Tanzania bara.

Kipindi cha kwanza Simba Sc ilifanikiwa kupata bao kupitia kwa Mzamiru na kuwapeleka mapumziko wakiwa mbele ya bao 1-0 huku Mtibwa akiwa nusu baada ya mchezaji wake Kitenge kupewa kandi nyekundu.

Kipindi cha pili Simba iliendelea kutoa dozi ya nguvu kwenye mchezo glhuo baada ya kuongeza mabao mengine na kufikia 5-0 huku Mtibwa tena akipewa kadi nyekundu mchezaji wake Cassian baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano.

Mabao ya Simba Sc mengine yamefungwa na Okra, Moses Phiri,Sakho ambaye amepachika mabao mawili kwenye mchezo huo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments