BIBI MWENYE JINO MOJA AENDELEA KUTINGISHA MITANDAO YA KIJAMII

Bibi kizee Mkenya anayefahamika kwa jina la Shosh Wa Kinangop amewafurahisha mashabiki wake kwa lugha ya mtaani ya shembeteng. TAZAMA Mambo yake  <HAPA>

Bibi huyo anayejaribu bahati yake katika ulimwengu wa mitandaoni kuunda maudhui hivi majuzi alijiunga na TikTok, na anapiga hatua kubwa.

Akiwa na video chache tu kwenye akaunti, amezidi likes 221k, ambapo ni mwanzo tu kwa mama huyo mkongwe. Mashabiki wake wanakisia kuwa huenda ni mmoja wa wajukuu zake wanaomsaidia kuendesha akaunti hiyo.

Akiwa amevalia sweta ya kijivu na kitambaa cha rangi ya samawati ya turquoise kichwani bibi huyo alionesha wazi hakuja kucheza mitandaoni. 

Aliwaambia mashabiki wake kwamba kwa sababu alikuwa mzee haimaanishi kuwa haelewi lugha ya vijana ya sheng.

 "Msinione mimi ni shosho, me najua sheng, nawalambotove."

'Shosh' ni jina la Kikuyu kumaanisha bibi au ajuza, na Kinangop ni eneo nchini Kenya anakotoka, kwa hivyo zinapowekwa pamoja inakuwa 'Shosh Wa Kinangop.

Haya ni baadhi ya maoni ya wafuasi wake;

@dinahmwenda933 alisema: "Lakini shosh ni mrembo na ni bayana alikuwa anang'aa siku zake za ujana....anapendeza."

@Delia poppy alisema: "Kila wakati naingia tik tok napatana na video zako zikiwa za kwanza shosh nifanyie video moja shosh."

@amazinghope0 alidokeza; "Kongole shosh, tunakupenda."

Hivi majuzi, bibi mmoja ambaye amekuwa kipenzi cha Wakenya wengi baada ya kuagiza kwa mzaha mafuta ya KSh 70,000 aliwafurahisha watu mitandaoni kwa kuzungumza kwa lugha ya sheng.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments