BILIONEA NAMBA MOJA DUNIANI RASMI AINUNUA TWITTER



BILIONEA namba moja duniani, Elon Musk amekamilisha ununuzi wake wake wa $44bn (£38.1bn) wa Twitter, kulingana na mwekezaji katika kampuni hiyo.


Mkurugenzi mkuu wa Twitter na bosi wa fedha wameripotiwa kuondoka mara moja.


Inaleta tamati sakata iliyoshuhudia Twitter ikienda mahakamani ili kumtaka tajiri huyo duniani kutii masharti ya mpango wa kutwaa umiliki wa kampuni hiyo baada ya kujaribu kutoroka.


Bw Musk alituma ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa nia yake kwenye jukwaa haikuwa kuhusu kupata pesa.


Mwekezaji wa Twitter Ross Gerber, ambaye ni afisa mkuu mtendaji wa Gerber Kawasaki Investments huko California, alithibitisha kwa BBC kwamba mpango huo umekamilika.


“Nadhani mahakama ilimsukuma juu sana ,” alisema Bw Gerber. “Kwa kweli, hii imekuwa janga tangu mwanzo, bila shaka, kuanza kwa ukali sana kwa Twitter kwa njia ambayo ililazimisha Twitter mezani … kisha kukasirika na kuwa na majibizano ya umma juu ya kile ambacho kwangu mimi kilijulikana’


Afisa mkuu Mtendaji wa kampuni hiyo, Parag Agrawal, na afisa mkuu wa fedha Ned Segal hawako tena na kampuni hiyo, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya Marekani.


Mwanzilishi mwenza wa Twitter Biz Stone alimshukuru Bw Agrawal, Bw Segal na afisa mkuu wa sheria na sera wa kampuni hiyo, Vijaya Gadde – ambaye pia anaripotiwa kuondoka kampuni hiyo – kwa “mchango wao mkubwa” katikakufanikisha mpango huo.


Hisa za mtandao huo wa kijamii zitasitishwa kufanya biashara siku ya Ijumaa, kulingana na tovuti ya New York Stock Exchange.


Bw Musk alisema alinunua jukwaa la mitandao ya kijamii kusaidia ubinadamu na alitaka “ustaarabu kuwa na eneo la kawaida la ukumbi wa kidijitali”.


Mapema wiki hii Bw Musk alitoa video inayomuonyesha akitembea katika makao makuu ya Twitter huko San Francisco akiwa amebeba sinki la jikoni na nukuu: “Acha hilo lizame!”


Pia alibadilisha wasifu wake wa Twitter ukasomeka “Chief Twit”.

Wachambuzi wengi walidai kuwa bei ambayo Bw Musk analipa kwa kampuni hiyo sasa ni ya juu sana kutokana na kushuka kwa thamani ya hisa nyingi za teknolojia na jitihada za Twitter kuvutia watumiaji na kukua.


Katika taarifa ya hivi majuzi ya mapato, mwanzilishi wa Tesla alisema Twitter ilikuwa “mali ambayo imedhoofika kwa muda mrefu, lakini ina uwezo wa ajabu, ingawa ni wazi mimi na wawekezaji wengine tunailipa zaidi Twitter hivi sasa”.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments