SIMBA SC YAENDELEA KUONESHA MAKALI YAKE, YAICHAPA KAGERA SUGAR 2-0



*********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Klabu ya Simba imefanikiwa kuondoka na alama tatu mbele ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa ligi Kuu NBC, mchezo ambao ulichezwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam
Simba Sc imeweza kupata mabao 2-0 ambayo yalifungwa na mastaa wao Moses Phiri pamoja na mshambuliaji wao Dejan Georgjevic.

Mpaka Mapumziko Simba Sc ilikuwa inaongoza kwa bao 1-0 ambalo lilifungwa baada ya Okrah kupiga mpira wa adhabu ambao ulimshinda goli kipa Kipao na Moses kufunga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments