MZEE MWENYE WATOTO 34 KUTOKA KWA WANAWAKE 20 AZUA GUMZO

Video ya mzee wa miaka 78 imeleta hisia mseto mitandaoni huku ikinasa ufichuzi wa kusisimua aliotoa kuhusu maisha ya jamii yake.

Mkulima huyo alifichua kuwa kwa sasa anaishi na mwanamke mwenye umri wa miaka 35 ambaye wamejaliwa watoto watano, amezaa watoto 34, lakini ni 32 pekee ambao wako hai.

Kulingana naye, watoto 20 kati yao ni wa mama 20 tofauti, na bado anaendelea kujifungua

Kwenye video iliyotamba mitandaoni mzee huyo aliwarai wanaume wengine kuufuata mfano wake akisema watoto ni baraka

Alipoulizwa kilichomsukuma kujifungua idadi kubwa ya watoto, mzee huyo alisema ‘utukufu’ wote ulitoka kwa Mungu kwa kumbariki.'

"Mke wangu wa sasa ana umri wa miaka 35 na tuna watoto watano lakini bado hatujamaliza kujifungua. Tutakuwa na wengine," alisema.

Prince Ko Fi alisema: "Mtu mmoja peke yake watoto 32 na serikali inapaswa kumsaidia kuwalipia wanawe karo ya shule. Ninaamini kunapaswa kuwa na idadi ya watoto ambayo mtu anapaswa kujifungua. Mtu mmoja anafaa kuwa na mtoto mmoja au wawili."


Shaibu Sahada alisema: "Anadhani hilo ni mzaha Lakini hii ni mojawapo ya matatizo ya Ghana. Angewezaje kulea watoto 32 ifaavyo? Watoto hao kuna uwezekano mkubwa wa kukosa malezi yoyote bora, na kwa pamoja wanakuwa mzigo kwa jamii nzima. Ni watu masikini tu ndio watafurahia kitu kama hiki."

Dyer Tsoeke alitaja: "Huyu hamshindi Togbe Asilenu ambaye ana watoto 100+. Kwa kweli Shaibu Sahada aliibua baadhi ya hoja halali ambazo tunapaswa kuzingatia kwa kina."


Katika hadithi sawa na hiyo, mwanaume aliyetambulika kwa jina la Nana ana watoto zaidi ya 200 na wake zake 43 katika Mkoa wa Juu Mashariki mwa Ghana.

Wafanyakazi wa Kipindi cha Asubuhi cha Angel TV (Anopa Bofo) wakiongozwa na Kofi Adomah walisafiri hadi Tenzuku, kijiji ambacho kiko umbali wa saa 13 kwa gari kutoka Accra, ili kuwahoji baadhi ya watoto kuhusu familia hiyo kubwa.

Ingawa mwanaume huyo mwenyewe hakuwepo, msemaji wake alionyesha kuwa makadirio ya idadi ya wake na watoto ilikuwa chini ya takwimu halisi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments