JINSI PICHA ZA UTUPU, VIDEO ZA NGONO ZINAPUNGUZA HAMU YA TENDO LA NDOA

Utandawazi na ongezeko la maarifa katika teknolojia ya vifaa ya mawasiliano umechangia kwa namna moja au nyingine kusambaa picha na video za ngono ambazo zinapatikana katika kanda za video, simu za mkononi na kwenye kompyuta zenye mtandao wa intaneti kwa gharama nafuu na wakati mwingine zinapatikana bure.

Wataalamu wa afya na saikolojia wanaeleza uraibu wa video za ngono ni moja kati ya sababu zinazochangia kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa, hasa kwa wanaume.

Inaelezwa kuwa mraibu wa picha za utupu anapokosa suluhisho la hisia zake kwa haraka anaweza kujikuta anajichua na akiendelea na tabia hiyo huweza kujikuta katika uraibu wa kitendo hicho hali inayosababisha kukosa hisia za kufanya tendo hadi atakapoangalia picha au video hizo. Pia anashindwa kudumu kufanya tendo la ndoa hadi aangalie picha au video za ngono.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments