UTAMADUNI WA WANAWAKE KUJIFUKIZA SEHEMU ZA SIRI KUWEKA MAMBO SAWA WASHIKA KASI....HILI NDIYO BALAA LAKE


Kushamiri kwa biashara ya urembo mtandaoni kumeleta bidhaa ambazo nyingine ni hatari kwa afya ya viungo vya uzazi kwa wanawake.

Bidhaa hizo za urembo zimeshamiri kutokana na matangazo yake na hasa madai ya uwezo wa kumtuliza mwenza pale mwanamke atakapoitumia kusafishia sehemu yake ya siri kwa njia ya kujifukiza na maji ya moto yaliyowekwa dawa hizo.

Mbali na kutumiwa kusafisha, pia zinadaiwa na wauzaji wa bidhaa hizo zinasaidia kupunguza ukubwa wa uke, kuondoa ukavu na kukaza misuli ya uke na hivyo kumvutia mwanamume.

Wafanyabiashara wa mtandaoni ndio wameiteka biashara hii inayohusisha mchanganyiko wa majani yanayoitwa ‘yoni steaming herbs’.


Kulingana na maelekezo ambayo yapo mitandaoni, majani haya huchemshwa na maji ya moto kisha maji hayo kuwekwa kwenye chombo ambacho kitaruhusu mvuke kutoka na mwanamke anachuchumaa au kukaa kwenye chombo hicho katika mtindo ambao umvuke utapita kwenye sehemu yake ya siri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments