BENKI YA CRDB KATIKA MAONESHO YA 46 YA SABASABA


Mgeni Rasmi katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Barani Afrika, Wankele Mene (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventure Paul, wakati alipotembelea banda hilo, katika ufunguzi rasmi wa maonesho hayo yanayaendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba, jijini Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji.
Mgeni Rasmi katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Barani Afrika, Wankele Mene (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Benki ya CRDB tawi la sabasaba, Angelita Msaki (kulia), pindi alipotembelea banda hilo, wakati wa ufunguzi rasmi wa maonesho hayo yanayaendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba, jijini Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji, akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventure Paul.
Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma (kushoto) akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayaendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba, jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Meneja wa Biashara wa Kanda ya Mashariki, George Yatera (katikati) pamoja na Meneja wa Benki ya CRDB tawi la sabasaba, Angelita Msaki.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya CRDB, Joseline Kamuhanda (kushoto) akizungumza na Meneja wa Benki ya CRDB tawi la sabasaba, Angelita Msaki, wakati wa maandalizi ya kumkaribisha Mgeni Rasmi wa Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Barani Afrika, Wankele Mene, katika banda lao.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya CRDB, Stephen Adili (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi wa Diaspora wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Bwana akiyetembelea banda la Benki ya CRDB katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), jijini Dar es salaam. Kulia ni Meneja wa Benki ya CRDB tawi la sabasaba, Angelita Msaki.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments