MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TATU AMUUA 'EX' WAKE DARASANI ALIVYOBAINI KAPATA MWANAUME MWINGINE


Shule ambayo mauaji yalifanyika

Polisi nchini Kenya wanamshikilia mwanafunzi wa kidato cha tatu aitwaye Tony Kiptoo (19) kwa kosa la kumuua kwa kumchoma na kisu wakiwa darasani aliyewahi kuwa mpenzi wake na wakaachana Irene Chelagat (22), baada ya kugundua amepata mwanaume mwingine na amemnunulia simu janja (Smartphone).


Vijana hao wawili wote walikuwa wakisoma katika shule ya sekondari Keben ya nchini humo na baada ya kuachana wote walikubaliana na kutakiana heri na ndipo Irene alipoanzisha mahusiano mengine.

Tukio la mauaji hayo limetokea Mei 4, 2022, baada ya kumchoma kisu hicho Irene kifuani na kupoteza maisha hapo hapo, tukio ambalo lilitokea kabla ya vipindi vya masomo vya asubuhi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments