WANAKIJIJI WAUA MAJAMBAZI WALIPORA MILIONI 1.2


Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi Mtatiro Kitinkwi
**
Majambazi wawili ambao majina yao hayajafahamika wameuawa na wananchi wilayani Kilwa mkoani Lindi, baada ya kuvamia duka la mfanyabiashara mmoja na kupora fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 1.2.


Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi Mtatiro Kitinkwi, amesema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 5, 2022, majira ya saa 2:00 usiku katika Kijiji cha Kisongo Pande wilayani kilwa mkoani humo.

"Watu hawa walikuwa wanne, wawili waliingia ndani na wawili walibaki nje na kupiga risasi juu ili kuwatisha wananchi na yule aliyevamiwa walioingia ndani walipora milioni 1.2, kutokana na Polisi Kata na ulinzi shirikishi wananchi waliweza kujikusanya na kuwadhibiti majambzai hao,"amesema Kamanda Kitinkwi.

CHANZO - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments