Post Top Ad
Saturday, May 14, 2022
SIMBA YATINGA NUSU FAINALI YA ASFC...YAIFUATA KIBABE YANGA
Na Alex Sonna
SIMBA w wametinga Nusu Fainali ya Michuano ya Kombe la Azam Sport Federation (ASFC) na kuifuata Yanga kibabe baada ya kuichapa mabao 4-0 Timu ya Pamba FC kutoka Mwanza Mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Simba yamefungwa na Peter Banda dakika ya 45 kipindi cha kwanza baada ya kupokea pasi ya Rally Bwalya bao lililopelekea Simba kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza bao moja.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko huku Simba ikinufaika zaidi na mabadiliko hayo.
Kibu Denis aliwanyanyua mashabiki wa Simba dakika ya 47 akifunga bao mara baada ya kupokea krosi ya Mohamed Hussein na mabaao mawili yamefungwa na Yusuph Mhilu dakika ya 52 na 88.
Kwa ushindi huo Simba watakutana na Yanga Nusu Fainali ya Michuano hiyo huku Azam FC watakutana na Coastal Union.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment