KUMTANIA MTU KUWA 'ANA UPARA' NI UNYANYASAJI WA KIJINSIA



Tony anadai alifanyiwa tukio hilo mwaka 2019.

Fundi umeme, Tony Finn aliyefanya kazi katika kampuni mmoja huko Uingereza kwa miaka 24 kabla ya kufukuzwa kazi mwezi Mei mwaka jana, aliifikisha mahakamani kampuni hiyo kwa unyanyasaji wa kijinsia.

Baada ya kufukuzwa kazi alimfungulia kesi bosi wake wa zamani, kwa madai aliwahi kumfanyia unyanyasaji wa kijinsia mwaka 2019 akiwa kazini kwa kumdhihaki muonekano wake hana nywele kichwani.

Aliipeleka kampuni hiyo mahakamani akidai amekuwa mwathirika wa unyanyasaji wa kijinsia baada ya kugombana na msimamizi wa kiwanda hicho, Jamie King.

Tony ameshinda kesi yake baada ya jaji wa mahakama Jonathan Brain, kutoa uamuzi kuwa, kumwita mtu ana upara ni unyanyasaji katika eneo la kazi kwa mujibu wa sheria za ajira nchini Uingereza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments