WATU WANNE WAFARIKI, 35 WAJERUHIWA AJALI YA BASI LA KILIMANJARO EXPRESS


Basi la Kilimanjaro Express lililopata ajali mkoani Songwe
Watu wanne wamefariki dunia huku wengine 35 wakijeruhiwa kufuatia ajali iliyohusisha basi la Kilimanjaro, linalofanya safari zake kutoka Tunduma kuelekea Dar es Salaam katika mlima Senjele mkoani Songwe.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Songwe Rashid Ngonyani, amesema kuwa ajali hiyo imetokea hii leo Machi 14, 2022, ambapo basi hilo lilitumbukia kwenye korongo na kuviringika mara kadhaa.

Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospitali ya Vwawa mkoani Songwe na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments