ANUSURIKA KUFA KWA KUPIGWA CHUMA KICHWANI NA MKEWE...AZINDUKA NA KUSAMEHE HOSPITALINI


Mwanamke aitwae Zainabu Mahomoka 35 ambaye ni Mkulima kutoka kijiji cha Makonjiganga Wilayani Liwale mkoa wa Lindi amenusurika kushitakiwa Mahakamani kwa kosa la kumjeruhi Mumewe aitwae Hemedi Nyanyweleka kwa kumpiga na chuma kichwani.

Tukio hilo lililotokea March 4 2022 mchana kutokana na ugomvi kati ya wanandoa hao huku chanzo kikielezwa kuwa ni ulevi uliopindukia wa Mume huyo ambako kulimpa hasira Zainabu na kumpiga Hemedi na chuma kichwani kulikomsababishia kupoteza fahamu.

Akiwa Hospitali baada ya kuzinduka Hemedi alipoelezwa kuwa Mke wake anatakiwa kufunguliwa mashtaka Mahakamani ili kujibu shitaka la kujeruhi…. Mwanaume huyu aliomba asipelekwe Mahakamani kujibu shtaka hilo kwani amemsamehe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments