MCHUNGAJI AUAWA KISA MILIONI MBILI


Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa, Elizabeth Amos, aliyeuawa

Jeshi la Polisi mkoa wa Iringa linamshikilia Naftali Lulandala, mkazi wa kijiji cha Uhambingeto kwa tuhuma za mauji ya mchungaji wa KKKT dayosisi ya Iringa  Elizabeth Amos, baada ya kuingia tamaa ya fedha na kumpora marehemu huyo kiasi cha shilingi milioni 2 kabla hajamuua.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa ACP Allan Bukumbi, amesema tukio hilo limetokea katika Kijiji cha Kipanduka wilayani kilolo mkoani Iringa ambapo marehemu alienda kwa ajili ya kufanya shughuli za usimamizi wa shamba wilayani humo.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments