JAMBAZI AJISALIMISHA POLISI...AAHIDI KUWA RAIA MWEMA




Mwanaume mmoja, Faida Komanya (34) mkazi wa Kijiji cha Bugalagala Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita ambaye alikuwa akituhumiwa na Jeshi la Polisi kwa kujihusisha na vitendo vya ujambazi, amejisalimisha kwa jeshi hilo na kuomba apelekewe kama raia mwema baada ya kujirekebisha tabia.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe, amesema mwanaume huyo amehusika katika matukio mengi ya kijambazi na aliwahi kufungwa katika Gereza la Butimba, Mwanza.

Kamanda Mwaibambe ameongeza kuwa kwa mujibu wa Komanya, ameamua kujisalimisha baada ya kupoteza ndugu wengi kwa kuuawa pamoja na kutengwa na ndugu wengine pamoja na jamii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments