MUIGIZAJI MAARUFU AMUUA DIRECTOR WAKE LOCATION WAKITENGENEZA FILAMU


Muigizaji maarufu kutoka nchini Marekani Alec Baldwin amemuua bila kukusudia Halyna Hutchins, ambaye ni muongozaji wa picha mjongeo (Director Of Photography) na kumjeruhi.

Joel Sauza ambae ni Director wa Filamu ya “RUST” kwa kutumia bunduki iliyoaminika kuwa ni bandia. Tukio hili limetokea New Mexico, Marekani walipokuwa kwenye eneo wakitengeneza (on set) filamu hiyo.

Hadi sasa Polisi wanaendelea na Uchunguzi na hamna aliyekamatwa. Alec Baldwin ameigiza kwenye filamu nyingi maarufu kama Concussion, The hunt for October, It’s Complicated.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments