MLEVI AZIKWA KWENYE JENEZA LA BIA..MWAMBA ALIPENDA SANA POMBE


Huko nchini Ghana kuna video inaendelea kusambaa mitandaoni ikimuonesha bwana mmoja akiwa kwenye jeneza lililoundwa kwa muonekano wa chupa ya bia.

Ingawa jina la mtu huyo halijawekwa wazi lakini inadaiwa mtu huyo alikuwa akipenda sana kunywa bia enzi za uhai wake na hivyo marafiki na jamaa zake katika kile wanachodai ni kumuenzi na kumuaga kwa heshima, wameamua kumtengenezea jeneza lenye mfanano na kile alichopenda kukinywa enzi za uhai wake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments