HOUSE GIRL AMFOKEA BOSI WAKE KWA KUMPIMIA CHAKULA.... 'NILIPOKUJA SIKUWA NIMEKONDA HIVI'


Kumezuka fujo ya aina yake katika nyumba moja eneo la Mlolongo Machakos nchini Kenya baada ya kijakazi 'House Girl' kumkaripia kwa ukali bosi wake kwa kumpimia chakula.

Kisa hicho kimejiri baada ya msichana huyo ambaye alikuwa amemfanyia kazi mwajiri wake kwa muda wa miezi mitano kudai kwamba bosi alikuwa na mazoea ya kumpimia chakula.

“Umenizoea sana,. Nilipokuja hapa sikuwa nimekonda hivi. Kila wakati umekuwa unanipimia chakula hata sishibi. Unanitesa sana,” Msichana huyo alisema. 

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mwajiri huyo anasemekana alikuwa na mazoea ya kumpimia dada huyo kiwango cha chakula ambacho alipaswa kukila asubuhi, mchana na jioni.

Duru zinaarifu kwamba kisanga hicho kiliwagutusha majirani kwani mrembo alikuwa akizungumza kwa sauti ya juu bila woga. 

“Kila asubuhi unaniambia nipike uji. Mchana ikifika unanipigia simu kuniambia ninunue chips ya KSh 30. Wewe ukiniangalia huu mwili wangu ni wa uji na chips?” mrembo aliwaka. 

Penyenye zinasema kuwa bosi aliamua kumzima dada huyo na vitisho vya kumfuta kazi.

 “Kama unaona chakula changu hakikutoshi nunua chako. Ukiendelea na huu ujinga wako walahi nitakufukuza,” mwenye nyumba alimuonya msichana huyo.

“Acha vitisho baridi. Wewe mwenyewe unajua mshahara unaonilipa ni mdogo. Kazi yako ni nyingi mno na chakula unanikazia. Unatakaje?” mrembo aliwaka. 

“Huu muda wote nimekufanyia kazi nimekuwa nikivumilia sana. Nimezoea kula ugali. Wewe hapa unanipimia chakula kama dawa ya kuua panya. Koma hiyo tabia,” meidi alimuonya bosi wake.

 Penyenye zinasema kwamba msichana huyo alitishia kutafuta kazi kwingine iwapo mwajiri wake hatakoma tabia hiyo. “Watu wengi sasa wanatafuta wasichana wa kazi. Hakuna haja ya kuendelea kukondeana hapa kwako,” msichana wa kazi alitisha.

 Duru zinaarifu kwamba bosi alipoona anazidi kuelemewa aliamua kufunga mdomo na kunyamza kama maji mtungini.

 “Kuanzia leo utanijua mimi ni nani. Nimevumilia sana. Nitakuwa nikila kulingana na kazi nitachapa la sivyo utabaki na kazi yako,” mrembo alisema.

CHANZO - TUKO NEWS

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments