RAIS SAMIA KUFANYA ZIARA YA KISERIKALI YA SIKU MBILI NCHINI RWANDA

 Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kiserikali ya siku mbili nchini Rwanda kuanzia Agosti 2, 2021 kwa mwaliko rasmi wa wa Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame

Akiwa Rwanda, Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na mengine atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, kisha atashuhudia utiaji saini hati za makubaliano na kuzungumza na vyombo vya habari

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu imeeleza kuwa ziara hiyo ya siku mbili inalenga kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano baina ya Rwanda na Tanzania.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments