KESI YA MBOWE NA WENZAKE YAAHIRISHWA HADI 13 AGOSTI 2021


Kesi ya ugaidi inayomkabili  Freeman Mbowe na wenzake 3 katika Mahakama ya Kisutu imeahirishwa hadi 13 Agosti 2021, baada ya upande wa Serikali kudai taratibu za kuifungua kesi hiyo katika Mahakama yenye mamlaka ya kuisikiliza kutokamlika.

Washtakiwa hao wamefikishwa Mahakamani hapo  leo Ijumaa, Agosti 6, 2021  asubuhi wakiwa kwenye basi dogo la Magereza likisindikizwa na magari mawili ya wazi yenye askari magereza wenye silaha za moto.

Baada ya kuwasili washtakiwa wote walishuka na kuelekea kwenye mahabusu ya Mahakama. Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Halfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Lingwenya.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments